Somo la 8/19

Ukurasa wa 1/3 Unaendeleaje? Tathmini na Marekebisho

Unaendeleaje? Tathmini na Marekebisho

Ujuzi unaotakiwa kutumika:

•  Kutafakari mchakato wa kujifunza kwako.

  Kutumia uzoefu wako kama mlezi.

 

Mada ya somo:

Katika somo hili la mafunzo utarejelea masomo ambayo umeshayakamilisha hadi sasa. Utatoa muhtasari wa kazi na uzoefu wako kabla ya kuendelea.

 

Malengo ya somo:

Lengo la somo ni kuakisi na mwalimu wako na wazazi walezi wengine kuhusu ulichokisoma na kufanikisha katika kazi yako, na namna mnavyoweza kufanya kazi pamoja vizuri zaidi.

 

“Somo hili lilitusaidia kuangalia maendeleo ya kila mtoto, kukagua, kukubali na kusaidia katika mtandao wetu wa kijamii, na jinsi ya kuendelea na kazi yetu. Tulikuwa na maoni mapya na kurekebisha namna tunavyofanya kazi pamoja”.

Kauli ya Mlezi

Tafadhali tumia dakika 15 (au muda mwingi kwa kadiri unavyohitajika) kwa ajili ya kuhitimisha ulichokifanyia kazi kati ya somo la mwisho na hili la sasa:

•  Je, ulifanikiwa kukamilisha kile ulichokipanga?
•  Nini kilikuwa rahisi kukifanya na kipi kilikuwa kigumu?
•  Je, ulijifunza nini kwa kufanya ulichokipanga?
•  Kipi utafanya vizuri zaidi wakati ujao katika masomo?

Tafadhali kumbuka: Haina shida kama ulipata matatizo-hii ndiyo namna mpya ya kufanya kazi, inahitaji kufanyia mazoezi kabla haujazoea.